|
|
|||||||
Alfagems Secondary School - Nafazi za MasomoMorogoro Tanzania ALFA = Auto Liberation For Africa |
||||||||
|
ALFAGEMS SECONDARY SCHOOL (S.3874) S.L.P. 6083 – MOROGORO Tel. 0765-899959 / 0713-784600 www.alfagems.com
Uongozi wa shule hii, inayozingatia taaluma na maadili kwa
kufuata sera ya elimu ya Kanisa Katoliki, unawashukuru nyinyi, wananchi wote,
kwa kuonyesha mmeipenda sana, na unafurahi kuwatangazia nafasi
zifuatazo: ·
KUJIANDAA KWA KIDATO CHA KWANZA (English
na Mathematics tu). Masomo yataanza tarehe 21 Septemba
2009 saa 8:00 mchana. Mwisho ni tarehe 18 Desemba 2009. Kufuata masomo hayo
hakumpi mwanafunzi haki yoyote ya kuchaguliwa asome kidato cha kwanza baadaye.
Ada ni Tsh. 30,000 tu. Wasichana wa bweni wataongeza Tsh. 90,000 tu. · KUSOMA
KIDATO CHA KWANZA (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology,
Chemistry, Physics na Mathematics tu). Usaili utafanyika kuanzia saa 2:00 asubuhi tarehe
24-10-2009, 21-11-2009 na 19-12-2009: kila mara watachaguliwa waliofanya
vizuri zaidi. Masomo yataanza tarehe 13 Januari 2010 saa 1:30 asubuhi. Ada ni
Tsh. 180,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). Wasichana wa bweni wataongeza Tsh.
260,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). ·
KUJIANDAA KWA MTIHANI WA MAARIFA (Q.T.
– Civics, History, Geography, English na Kiswahili tu). Masomo
yataanza tarehe 19 Oktoba 2009 saa 8:00 mchana (watasoma Jumamosi asubuhi
pia). Ada ni Tsh. 160,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). Wasichana wa bweni
wataongeza Tsh. 340,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). ·
KUSOMA
KIDATO CHA TATU NA CHA NNE KWA MWAKA MMOJA (Civics, History, Geography,
English na Kiswahili tu). Wanaotaka kujiunga wanahitaji kuwa wamefaulu
mtihani wa maarifa (QT) au wamefanya ule wa kidato cha nne. Masomo yataanza
tarehe 19 Oktoba 2009 saa 8:00 mchana (watasoma Jumamosi asubuhi pia). Ada ni
Tsh. 160,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). Wasichana wa bweni wataongeza Tsh.
340,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). ·
KUJIANDAA KURISITI MTIHANI WA KIDATO
CHA NNE (Civics, History, Geography, English Kiswahili na Bible tu; au Civics,
Geography, English, Literature na Kiswahili tu; au Civics, History, Geography,
English tu; au History, Geography na Literature tu; au Civics, Kiswahili na
Bible tu; au Biology na Mathematics tu). Masomo yataanza tarehe 8
Februari 2010 saa 8:00 mchana (watasoma Jumamosi asubuhi pia). Ada ni Tsh.
100,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). Wasichana wa bweni wataongeza Tsh.
220,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). ·
KUSOMA KIDATO CHA TANO (HKL na HGK). Wanaotaka
kujiunga wanahitaji kuwa wamepata tayari credits tatu katika masomo yoyote.
Wawe pia wamepata walau D katika somo la English. Masomo yataanza tarehe 12
Aprili 2010 saa 1:30 asubuhi. Ada ni Tsh. 200,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne).
Wasichana wa bweni wataongeza Tsh. 260,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). · KUSOMA
KIDATO CHA TANO NA CHA SITA KWA MWAKA MMOJA (HKL na HGK). Wanaotaka
kujiunga wanahitaji kuwa na credits tatu tayari katika masomo yoyote
walipofanya au kurisiti mtihani wa kidato cha nne. Wawe pia wamepata walau D
katika somo la English. Masomo yataanza tarehe 8 Februari 2010 saa 8:00 mchana
(watasoma Jumamosi asubuhi pia). Ada ni Tsh. 260,000 tu kwa mwaka (mikupuo
minne). Wasichana wa bweni wataongeza Tsh. 340,000 tu kwa mwaka (mikupuo minne). Kwa Wakristo wa madhehebu yoyote somo
la Bible Knowledge au la Divinity ni la lazima. Kwa wengine ni la hiari. Ili kukwepa ulanguzi, fomu za kujiunga
zinapatikana hapa tu kwa Tsh. 10,000 na zinakuwa batili wiki moja baada ya
masomo kuanza. Ile ya kidato cha kwanza inaweza
kununuliwa hata siku ya usaili, mradi mhusika alete picha yake. Shule haina nafasi katika kidato cha
pili, cha tatu, cha nne na cha sita. Tafadhalini, mzingatie taratibu hizi,
kwa sababu msongo ni mkubwa mno: ndiyo sababu tunalazimika kuchuja
sana. Kila mtu aelewe kwamba taaluma inadai idadi ya wanafunzi
darasani isizidi kiwango fulani. Kutaka kijana apokewe nje ya taratibu
zilizopangwa ni kuwadhuru kielimu
waliokwishakubaliwa.
|
||||||||
| Copyright © 2009 Alfagems Co. ltd Morogoro Tanzania | ||||||||