Jimbo Katoliki la Morogoro Mashirika

Mashirika

Vito mbalimbali katika taji la dhahabu ambalo Kristo amempamba Bibiarusi wake. Au fungu zuri la maua ya kila rangi. Ni mifano miwili iliyotumika kuelezea wingi wa mashirika ya kitawa ndani ya Kanisa Katoliki. Jimbo la Morogoro ni mojawapo kati ya yale yanayofurahia zaidi neema kubwa namna hiyo.

Tukirudi nyuma hadi karne ya XIX , tunakuta kwamba watawa wa Roho Mtakatifu (Holy Ghost Fathers) ndio waanzilishi wenyewe wa Kanisa nchini, wakitokea Zanzibar na Bagamoyo, na kufuatwa muda si mrefu baadaye na masista kutoka kisiwa cha Réunion (Filles de Marie) Hivyo tangu awali watawa wamekuwa mstari wa mbele sio tu katika maisha ya Kiroho, bali pia katika umisionari.

Mwanzo mgumu: kwa miaka mingi mashirika hayo yaliinjilisha wakistahimili tabu na hari za mchana, mpaka watawa wengine hasa wananchi, tunda la kazi yao, wakaja kuwaunga mkono kwa saa tofautitofauti.

Masista wengi wa nchi nzima wanafahamu sana jimbo hili kwa sababu waliwahi kusoma Bigwa, katika sekondari iliyoanzishwa kwa ajili yao na Umoja wa Mama Wakuu Tanzania (ambao kwa sasa unakamilisha ujenzi wa kituo kingine cha malezi ya pamoja si mbali na shule hiyo).

Hatua mpya ya uwepo wa mashirika jimboni ilipigwa pale ambapo Wasalvatoriani kisha kupatana na mashirika mengine walichagua Morogoro kama mahali pa kujenga seminari kuu ya kitawa ambayo kwa sasa ni Taasisi ya Falsafa na Tauhidi (wengine wanafikiria kuigeuza tena iwe Chuo Kikuu chenye vitivo mbalimbali). Hayati Askofu Adriani Mkoba alifungua milango ya jimbo kulipokea kila shirika litakalohitaji watawa wake wasomee huko. Tangu hapo ujenzi na malezi havijakoma katika eneo la mlima Kola, kwenye barabara ya Dar es Salaam. Yeyote anayepita anajionea maendeleo hayo na kuzungumzia aina hiyo ya Vatikano chini ya milima ya Uluguru.

Mvuto wa taasisi hiyo ndio sababu kuu ya mashirika kumiminika Morogoro miaka ya mwisho; lakini ukianza kuelekea Dodoma, kwenye eneo la Kihonda unakuta vilevile mashirika mengi, ingawa majengo yao yamefichikafichika kati ya nyumba za wananchi.

Kwa jumla sasa hivi jimbo lina mashirika zaidi ya 30 ya kila aina: ya wanaume na ya wanawake, ya kikleri na ya kilei, ya maisha ya wakfu na ya maisha ya kitume, ya kipapa na ya kijimbo. Inakosekana bado monasteri ya maisha ya sala tu, ingawa Askofu Telesphor Mkude ana hamu nayo.

Mhashamu akiona kwa furaha kubwa ongezeko hilo ambalo linaendelea haraka, mwanzoni mwa Jubilei kuu ya mwaka 2000, pamoja na kumteua kwa mara ya kwanza makamu wake maalumu kwa maisha ya wakfu aliamua kuunganisha mashirika hayo yote katika ASSICAL (Association of Institutes of Consecrated and Apostolic Life – Morogoro Diocese) ili yaweze kufahamiana na kubadilishana mawazo, mang’amuzi, matarajio na mipango hasa upande wa malezi na wa utume.

Tangu hapo utume huo unazidi kuimarika kwa njia ya mikutano na adhimisho la pamoja la sikukuu ya watawa iliyoanzishwa na Papa Yohane Paulo II kwenye tarehe 2 Februari ya kila mwaka. Kwa kweli ni tukio la kufurahisha kuona mamia ya watawa wa mabara karibu yote kushangilia miito yao mbalimbali kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Lakini siku moja haiundi mwaka. Kuna siku nyingine 364 ambazo ni nafasi ya kila mtu kumshukuru Mungu kimatendo kwa karama aliyomjalia. Uaminifu wa kila sasa ndio unaothibitisha kwamba neema inapokewa kwa mikono miwili badala ya kuchezewa. La sivyo adhimisho halina maana. Changamoto hiyo ipo daima mbele ya kila mmoja na ya kila jumuia, kwa sababu maisha ya kitawa ni ya kulenga utakatifu pamoja na wengine, sio kibinafsi.

Mbali ya utakatifu, mashirika yanalenga kutoa mchango katika Kanisa na katika jamii, kila moja kadiri ya karama yake. Ingawa nguvu nyingi za mashirika mbalimbali yaliyohamia jimboni kwa ajili ya malezi zinaishia katika kazi hiyo ya msingi, tunaweza kusema nia ya kufanya kitu hata nje ya nyumba ipo. Kadiri ushirikiano unavyostawi, njia zinaonekana, kwa sababu penye nia pana njia.

Mahitaji ya jimbo hasa ni mengi, kama kawaida. Hivyo mapadri na walei wanatazamia sana kufaidika na uwepo wa umati huo wa waamini wenzao waliojitoa kabisa kwa maisha ya wakfu na ya kitume. Baadhi ya mashirika yana nyumba zisizo za malezi, nazo ndizo zinazoitikia zaidi mahitaji hayo. Kwa namna ya pekee Masista wa Moyo Safi wa Maria wa Morogoro, ambao ndio wengi, wanahudumia parokia, shule na zahanati nyingi jimboni kote.

Mungu atujalie sisi sote kushika kwa unyenyenyeku nafasi aliyotupangia katika kufikisha watu kwenye uzima wa milele.  

1. MASHIRIKA YA MAISHA YA WAKFU

 

1.1. Mashirika ya Kitawa

 

1.1.1. Ya Kiume

 

1.      Ndugu Wafransisko Wakonventuali - SLP 932 - Morogoro

Simu: +023/0784594072 - Barua pepe: krzcie@yahoo.com - Tovuti: www.ofmconv.org

2.      Ndugu Wafransisko Wakapuchini - SLP 900 - Morogoro

Simu: +023/2603204 - Barua pepe: kolafriars@yahoo.com - Tovuti: www.ofmcap.org

3.      Ndugu Waagustino - SLP 1947 - Morogoro

Simu: +023/2604773 - Barua pepe: osamorogoro@yahoo.com - Tovuti:

4.      Wakarmeli OCD - SLP 363 - Morogoro

Simu: +023/2603800 - Barua pepe: ocdtzmission@yahoo.com - Tovuti:

5.      Shirika la Roho Mtakatifu - SLP 16 - Bagamoyo

Simu: +023/2440063 - Barua pepe: eap@habari.co.tz - Tovuti:

6.      Wamisionari wa Mt. Francis wa Sales - SLP 12 - Morogoro

Simu: +023/2600036 - Barua pepe: msfsmoro@africaonline.co.tz - Tovuti: www.fransalians.com

7.      Shirika la Madonda Matakatifu (Wastigmatini) - SLP 2213 - Morogoro

Simu: +023/2603523 - Barua pepe: stigmatines@morogoro.net - Tovuti: www.stigmatines.com

8.      Wamisionari Wana wa Moyo Safi wa Maria (Waklareti) - SLP 427 - Morogoro

Simu: +023/2600429 - Barua pepe: cmfmorobarbastro@yahoo.com - Tovuti: www.claret.org

9.      Wasalvatoriani - SLP 1878 - Morogoro

Simu: +023/2600897 - Barua pepe: sdsschol@go2.pl - Tovuti: http://www.sds-ch.ch/africa

10.  Wamisionari wa Consolata - SLP 769 - Morogoro

Simu: +023/2603563 - Barua pepe: allasemi@morogoro.net - Tovuti: http://www.consolata.org

11.  Shirika la Misheni (Wavinsenti) - SLP 6051 - Morogoro

Simu: +023/2600029 - Barua pepe: depaulmoro04@yahoo.com - Tovuti:

12.  Mabradha wa Elimu ya Kikristo wa Mt. Gabrieli (Wamontfort) - SLP 1124 - Morogoro

Simu: +023/2602204 - Barua pepe: montmoro@africaonline.co.tz - Tovuti:

 

 

1.1.2. Ya Kike

 

1.      Mabinti wa Maria (wa St. Denis)- SLP 230 - Bagamoyo

Simu: 023/2440417 - Barua pepe: dmdestdenistan@yahoo.fr - Tovuti:

2.      Masista Wamisionari wa Damu Takatifu - SLP 865 - Morogoro

Simu: +023/2604655 - Barua pepe: - Tovuti:

3.      Shirika la Moyo Safi wa Maria (wa Morogoro) - SLP 1049 - Morogoro

Simu: +023/2603591/2604314 - Barua pepe: mgololesisters@intafrica.com - Tovuti:

4.      Masista wa Msalaba Mtakatifu (wa Chavonod)- SLP 1677 - Morogoro

Simu: +023/2603328 - Barua pepe: holycross@africaonline.co.tz - Tovuti:

5.      Masista Watersiari Wakapuchini wa Familia Takatifu - SLP 1989 - Morogoro

Simu: +023/2604845 - Barua pepe: htctanz@hotmail.com - Tovuti:

6.      Masista wa Mt. Anna (wa Luzern) - SLP 1807 - Morogoro

Simu: +023/2601550 - Barua pepe: stannsmoro@africaonline.co.tz - Tovuti:

7.      Masista Wakolejina wa Familia Takatifu - SLP 945 - Morogoro

Simu: +023/2600424 - Barua pepe: collemoro@hotmail.com - Tovuti:

8.      Masista wa Maria Imakulata (wa Krishnagar) - SLP 2028 - Morogoro

Simu: +023/2604066 - Barua pepe: smimoro@africaonline.co.tz - Tovuti:

9.      Masista wa Mama wa Karmeli - SLP 1302 - Morogoro

Simu: +023/2600359 - Barua pepe: - Tovuti:

10. Masista wa Mt. Gemma - SLP 304 - Morogoro-

Simu: +0784/457358 - Barua pepe: - Tovuti:

11. Masista Waursula wa Yesu Mteswa - SLP 1048 - Morogoro

Simu: +0756/937297 - Barua pepe: - Tovuti:

12. Masista wa Sakramenti Kuu - SLP 2135 - Morogoro

Simu: +023/2602902 - Barua pepe: - Tovuti:

13. Mabinti wa Mt. Fransisko wa Sales – SLP 640 - Morogoro

Simu: +023/2600900 - Barua pepe: dsfstanzania@rediffmail.com - Tovuti:

14. Masista wa Maria Imakulata (wa Wroclaw) - SLP 1878 - Morogoro

Simu: +0787/759496 - Barua pepe: - Tovuti:

15. Masista wa Mt. Yosefu (wa Annecy) - SLP 58 - Dumila

Simu: +0745/214343 - Barua pepe: agnesadampukulam@yahoo.com - Tovuti: www.sisters of st.joseph of Annecy

16. Masista wa Mt. Yosefu (wa Chambery) - SLP 135 – Mikumi

Simu: +0787/710338 - Barua pepe: - Tovuti: www.csjchambery.org

17. Masista wa Bikira Maria Malkia wa Mitume - SLP 1925 - Morogoro

Simu: +023/2604165 - Barua pepe: - Tovuti:

18. Masista wa Mt. Anna (wa Bangalore) – SLP 363 – Morogoro

Simu: +023/603800 - Barua pepe: - Tovuti:

19. Masista Waabuduo Damu ya Kristo – SLP 6508 – Morogoro

Simu: - Barua pepe: - Tovuti:

20. Dada Wadogo wa Mt. Fransisko – SLP 1878 – Morogoro

Simu: +0787/759496 - Barua pepe: - Tovuti:

21. Masista Wabenedikto Waafrika wa Mt. Agnes – SLP 6015 – Morogoro

Simu: +0784/464024 - Barua pepe: mlowevicky@yahoo.com - Tovuti:

22. Masista wa Mt. Karolo Borromeo – SLP 1232 – Morogoro

Simu: +0732/931181 - Barua pepe: - Tovuti:

23. Masista Warosmini wa Maongozi – SLP 133 – Morogoro

Simu: +0787/024621 - Barua pepe: - Tovuti:

 

 

 

1.2. Mashirika ya Kilimwengu

 

1.2.1. La Kiume

 

1.      Mapadri wa Shirika la Kilimwengu katika Kazi ya Roho Mtakatifu – SLP 640 – Morogoro

Simu: +023/2603340 - Barua pepe: - Tovuti:

 

 

1.2.2. Ya Kike

 

1.      Unitas kwa Afrika - SLP 1003 - Morogoro

Simu: +023/2600138 - Barua pepe: - Tovuti:

2.      Masista wa Grail - SLP 6090 - Morogoro

Simu: +023/2613690 - Barua pepe: - Tovuti:

 

 

 

2. MASHIRIKA YA MAISHA YA KITUME

 

2.1. Ya Kiume

 

1.      Wamisionari wa Damu Azizi - SLP 1925 - Morogoro

Simu: +023/2604165 - Barua pepe: stgascoll @yahoo.com - Tovuti: www.cpps-preciousblood.org

2.      Jumuia ya Mapadri katika Kazi ya Roho Mtakatifu - SLP 1935 - Morogoro

Simu: +023/2601353 - Barua pepe: - Tovuti:

 

 

2.2. La Kike

 

1.      Jumuia ya Masista katika Kazi ya Roho Mtakatifu - SLP 6038 - Morogoro

Simu: +023/2601764 - Barua pepe: - Tovuti:

 

 

 

3. TAASISI ZA MALEZI YA PAMOJA KATI YA MASHIRIKA YA KIKE

 

1.      Sekondari ya Masista ya Bigwa - SLP 369 - Morogoro

Simu: +023/2603066 - Barua pepe: bigwasrs@yahoo.com - Tovuti:

2.      Kituo cha Malezi ya Masista cha Kola – SLP 913 – Morogoro

Simu: +023/2600658 - Barua pepe: tcastanzania@hotmail.com - Tovuti:

 

 

 

4. CHAMA (CHA WANAUME NA WANAWAKE)

 

1.      Ndugu Wadogo wa Afrika - SLP 6083 - Morogoro

Simu: - Barua pepe: unwa@unwa.tk Tovuti: www.unwa.tk

 

 

 

 

 

 

 

1. INSTITUTES OF CONSECRATED LIFE

 

1.1. Religious Institutes

 

1.1.1. Of men

 

1.      Friars Minor Conventual - P.O.Box 932 - Morogoro

Phone: +023/0784594072  - E-mail: krzcie@yahoo.com - Website:

2.      Friars Minor Capuchin - P.O.Box 900 - Morogoro

Phone: +023/2603204 - E-mail: kolafriars@yahoo.com - Website:

3.      Augustinian Friars - P.O.Box 1947 - Morogoro

Phone: +023/2604773 - E-mail: osamorogoro@yahoo.com - Website:

4.      Discalced Carmelites - P.O.Box 363 - Morogoro

Phone: +023/2603800 - E-mail: ocdtzmission@yahoo.com - Website:

5.      Holy Ghost Fathers- P.O.Box 16 - Bagamoyo

Phone: +023/2440063 - E-mail: eap@habari.co.tz - Website:

6.      Missionaries of St. Francis of Sales - P.O.Box 12 - Morogoro

Phone: +023/2600036 - E-mail: msfsmoro@africaonline.co.tz - Website: www.fransalians.com

7.      Stigmatines - P.O.Box 2213 - Morogoro

Phone: +023/2603523 - E-mail: stigmatines@morogoro.net - Website: www.stigmatines.com

8.      Claretians - P.O.Box 427 - Morogoro

Phone: +023/2600429 - E-mail: cmfmorobarbastro@yahoo.com - Website: www.claret.org

9.      Salvatorians - P.O.Box 1878 - Morogoro

Phone: +023/2600897 - E-mail: sdsschol@go2.pl - Website: http://www.sds-ch.ch/africa

10.  Missionaries of Consolata - P.O.Box 769 - Morogoro

Phone: +023/2603563 - E-mail: allasemi@morogoro.net - Website: http://www.consolata.org

11.  Congregation of Mission (Vincentians) - P.O.Box 6051 - Morogoro

Phone: +023/2600029 - E-mail: depaulmoro04@yahoo.com - Website:

12.  Montfort Brothers of the Christian Instruction of St. Gabriel - P.O.Box 1124 - Morogoro

Phone: +023/2602204 - E-mail: montmoro@africaonline.co.tz - Website:

 

 

1.1.2. Of women

 

1.      Daughters of Mary (of St. Denis)- P.O.Box 230 - Bagamoyo

Phone: +023/2440417 - E-mail: dmdestdenistan@yahoo.fr - Website:

2.      Missionary Sisters of the Precious Blood - P.O.Box 865 - Morogoro

Phone: +023/2604655 - E-mail: - Website:

3.      Immaculate Heart of Mary Sisters (of Morogoro) - P.O.Box 1049 - Morogoro

Phone: +023/2603591/2604314 - E-mail: mgololesisters@intafrica.com - Website:

4.      Holy Cross Sisters (of Chavonod)- P.O.Box 1677 - Morogoro

Phone: +023/2603328 - E-mail: holycross@africaonline.co.tz - Website:

5.      Capuchin Tertiary Sisters of the Holy Family - P.O.Box 1989 - Morogoro

Phone: +023/2604845 - E-mail: htctanz@hotmail.com - Website:

6.      Sisters of St. Ann (of Luzern) - P.O.Box 1807 - Morogoro

Phone: +023/2601550 - E-mail: stannsmoro@africaonline.co.tz - Website:

7.      Collegine Sisters of the Holy Family - P.O.Box 945 - Morogoro

Phone: +023/260424 - E-mail: collemoro@hotmail.com - Website:

8.      Sisters of Mary Immaculate (of Krishnagar) - P.O.Box 2028 - Morogoro

Phone: +023/2604066 - E-mail: smimoro@africaonline.co.tz - Website:

9.      Sisters of Mother of Carmel - P.O.Box 1302 - Morogoro

Phone: +023/2600359 - E-mail: - Website:

10. Sisters of St. Gemma - P.O.Box 304 - Morogoro-

Phone: +0784/457358 - E-mail: - Website:

11. Ursuline Sisters of the Agony of Jesus - P.O.Box 1048 - Morogoro

Phone: +0756/937297 - E-mail: - Website:

12. Blessed Sacrament Sisters - P.O.Box 2135 - Morogoro

Phone: +023/2602902 - E-mail: - Website:

13.  Daughters of St. Francis de Sales - P.O.Box 640 - Morogoro

Phone: +023/2600900 - E-mail: dsfstanzania@rediffmail.com - Website:

14.  Sisters of Mary Immaculate (of Wroclaw) - P.O.Box 1878 - Morogoro

Phone: +0787/759496 - E-mail: - Website:

15.  Sisters of St. Joseph (of Annecy) - P.O.Box 58 - Dumila

Phone: +0745/214343 - E-mail: agnesadampukulam@yahoo.com - Website: www.sisters of st.joseph of Annecy

16.  Sisters of St. Joseph (of Chambery) - P.O.Box 135 - Mikumi

Phone: +0787/710338 - E-mail: - Website: www.csjchambery.org

17.  Sisters of Mary Queen of the Apostles - P.O.Box 1925 - Morogoro

Phone: +023/2604165 - E-mail: - Website:

18.  Sisters of St. Ann (of Bangalore) - P.O.Box 363 - Morogoro

Phone: +023/603800 - E-mail: - Website:

19.  Adorers of Blood of Christ - P.O.Box 6508 - Morogoro

Phone: - E-mail: - Website:

20.  Little Sisters of St. Francis of Assisi - P.O.Box 1878 - Morogoro

Phone: +0787/759496 - E-mail: - Website:

21.  African Benedictine Sisters of St. Agnes - P.O.Box 6015 - Morogoro

Phone: +0784/464024 - E-mail: mlowevicky@yahoo.com - Website:

22.  Sisters of St. Charles Borromeo - P.O.Box 1232 - Morogoro

Phone: +0732/931181 - E-mail: - Website:

23.  Rosminian Sisters of Providence - P.O.Box 133 - Morogoro

Phone: +0787/024621 - E-mail: - Website:

 

 
 
 

1.2. Secular Institutes

 

1.2.1. Of men

 

1.      Secular Institute of Priests in Opus Spiritus Sancti - P.O.Box 640 - Morogoro

Phone: +023/2603340  - E-mail: - Website:

 

 

1.2.2. Of women

 

1.      Unitas for Africa - P.O.Box 1003 - Morogoro

Phone: +023/2600138 - E-mail: - Website:

2.      The Grail - P.O. Box 6090 - Morogoro

Phone: +023/2613690 - E-mail: - Website:

 

 

 

 

1.      SOCIETIES OF APOSTOLIC LIFE

 

2.1. Of men

 

1.      Missionaries of the Precious Blood - P.O.Box 1925 - Morogoro

Phone: +023/2604165 - E-mail: stgascoll @yahoo.com - Website: www.cpps-preciousblood.org

2.   Apostolic Life Community of Priests in Opus Spiritus Sancti - P.O.Box 1935 - Morogoro

Phone: +023/2601353 - E-mail: - Website:

 

 

2.2. Of women

 

1.      Apostolic Life Community of Sisters in Opus Spiritus Sancti - P.O.Box 6038 - Morogoro

Phone: +023/2601764 - E-mail: - Website:

 

 

 

3. INTERCONGREGATIONAL CENTRES OF FORMATION FOR SISTERS

 

1.   Bigwa Sisters’ Secondary School - P.O.Box 369 - Morogoro

Phone: +023/2603066 - E-mail: bigwasrs@yahoo.com - Website:

2.   Kola Sisters’ Holistic Formation Centre - P.O.Box 913 - Morogoro

Phone: +023/2600658  - E-mail: tcastanzania@hotmail.com - Website:

 

 

 

4. ASSOCIATION (OF MEN AND WOMEN)

 

1.      Little Brothers and Sisters of Africa - P.O.Box 6083 - Morogoro

Phone: - E-mail: unwa@unwa.tk - Website: www.unwa.tk.