Historia
|
![]() |
Historia
kwa ufupi (ya jana na ya kesho)
Ndugu
Wadogo wa Afrika walianza kukusanyika tarehe 4-10-1991 kwenye kijiji cha Izazi (mkoa
wa Iringa, nchini Tanzania), halafu wakahamia Mkungugu (mkoa huohuo) na kuanzia
tarehe 31-10-1995 katika mtaa mmojawapo wa mji wa Morogoro.
Muda
wa jaribio ulimalizika tarehe 9-7-1997, askofu Telesphor Mkude wa Morogoro
alipounda rasmi chama chao pamoja na kuthibitisha katiba yake.
Wakati
wa adhimisho la ekaristi waanzilishi 11 (6 wa kike na 5 wa kiume) waliweka ahadi
ya kuishi kijumuia Injili kadiri ya Kanuni ya Utawa Hasa wa Tatu wa mtakatifu
Fransisko, iliyothibitishwa na papa Yohane Paulo II, na kadiri ya katiba hiyo
maalumu.
Baada
ya nyumba asili mbili, ziliongezeka ile ya kiume ya Kiroka (27-1-1998), ile ya
kike ya kijiji hichohicho (15-9-1998) na ile ya kiume ya Langali (10-7-2000),
zote zikiwa katika mkoa wa Morogoro.
Tangu
tarehe 4-11-2004 wameanza kuwepo
hata Kapelekesi katika jimbo la Mbeya, mipakani kwa Malawi.
Mnamo tarehe7 Januari 2007 waliowekwa wakfu kwa ahadi ya daima walikuwa 11 (6 wa kiume na 5 wa kike), wanachama wenye ahadi ya muda walikuwa 17 (5 kwa 12), na ndugu kwenye jaribio 16 (6 kwa 10).
Hamu kuu ya ndugu hao ni
kumshuhudia Yesu kwa maneno na kwa maisha yao yote, katika Afrika nzima na mpaka
miisho ya dunia, kwa kuwa
kila mtu anamhitaji yeye, mwokozi
wa ulimwengu, na kwa hiyo ana haki ya kumjua ili awe kitu kimoja naye na Baba
aliyemtuma.
Kwa ajili hiyo wanatarajia kupata
mapema Wafransisko wa ulimwenguni, hasa wenye ndoa, ambao washuhudie tunu
zilezile za kwao katika maisha ya kila siku ya watu wa kawaida: katika familia,
uchumi, siasa n.k.